Jumapili, 6 Novemba 2016

Visima kumi na sita vya mafuta vyachomwa na IS Mosul

wanamgambo wa IS walioachia eneo la kusini ya Mosul nchini Iraq wamechoma moto visima vya mafuta kumi na tisa.

Mwandishi wa BBC kutoka eneo hilo anasema kuwa watu wengi wanaosumbuliwa na matatizo ya kupumua na wanyama wamekufa.

Uchafuzi wa mazingira kutokana na kuungua kwa visima hivyo vya mafuta kumesababisha mifugo kuwa na rangi nyeusi.

I-S bado wanadhibiti visima vya mafuta takribani sita nje ya Mosul na kuna hofu kwamba wanamgambo wake wanaweza kuchoma moto kwa visima hivyo pia.

Vikosi vya Serikali ya Iraq vimekua vikifanya jitihada katika siku za karibuni ili kukomboa mji wa Mosul kutoka kwa I-S.

MILINDIMO YA UCHAGUZI MAREKANI

Mkurugenzi wa FBI,James Comey ameliambia bunge la Marekani kuwa baada ya kupitia barua pepe zilizogundulika kutoka kwa Hillary Clinton, wakati alipokua waziri wa mambo ya nje wamegundua kuwa hana hatia yoyote na hawatamfungulia mashtaka.

Kampeni za Clinton ziliingia doa wiki iliyopita baada ya mkurugenzi huyo wa FBI kusema kuwa watazipitia barua pepe zake zilizopatikana katika kompyuta ya msidizi wa zamani wa mume wake.

Kauli hiyo imeonekana kumfurahisha mkuu wa mawasiliano wa kampeni za Clinton Jennifer Palmieri

Wakati upande wa Bi Clinton wakifurahia hatua hiyo kwa upande wake Donald Trump amesema Hillary Clinton analindwa na mfumo wa wizi wa kura, amesema Bi Clinton angetakiwa kuchunguzwa kwa muda mrefu.

Na hivi sasa tunaunana moja kwa moja na Zuhura ebu tuambie baada ya FBI kusema hawatamshtaki Hilary Clinton, hali ikoje kwa sasa ikiwa ndio imebaki takribani siku moja uchaguzi ufanyike.

NEW SONG

Free watch out new song of Raynavy called sugu through open up the link bellow.
WATCH NOW

Punguza unene kwa haraka.

Namna rahisi na salama ya kupunguza unene

Ukizungumza na watu wengi wanene wanataka kujua njia ya kupunguza mafuta tumboni. Njia rahisi na salama ya kupunguza mafuta katika tumbo au kitambi ni ile ya kupangilia chakula na kufanya mazoezi.

Kama unataka kupunguza tumbo kwa haraka basi punguza kula vyakula vyenye wanga na badala yake tumia mbogamboga na matunda kwa wingi.

Vyakula kama viazi mviringo, wali, mkate hukaa tumboni kwa zaidi ya siku tatu, pia ulaji wa nyama nyekundu unasababisha kuongezeka uzito na pia huongeza ukubwa wa tumbo.

Vyakula hivyo vinatakiwa kutumiwa kwa kiasi kidogo sana. Kuna wakati tumbo linajitokeza na kuwa kubwa kuliko kawaida hali hiyo inasababishwa na kula vyakula vya wanga kwa wingi, kutokunywa maji ya kutosha na pia kula bila ya mpangilio maalum.
Vyakula vya wanga na mafuta hufanya mtu kunenepa, acha au kupunguza kula vyakula hivyo.

Tumbo kuwa kubwa ni dalili kuwa chakula unachokula hakifanyi kazi inayotakiwa, kumekuwa na ziada mwilini na hii ziada inafanyika mafuta ambayo hujiwekesha akiba katika maeneo mbalimbali ya mwili.

Kwa kuwa chakula hiki cha ziada huwa hakitakiwi, mwili hukibadilisha na kuweka akiba katika mfumo wa mafuta kitaalam kama glycogem.

Unaweza kukabiliana na kuzidi kwa protini zinazoyeyushwa na kuwekwa katika akiba kwa mfumo huo wa mafuta. Mtu mwenye tatizo hilo ni bora akapangilia mlo wake kwa siku kama ifuatavyo.

Asubuhi pata kifungua kinywa kilichokamilika, pata mlo wa mchana kama kawaida na usiku kula matunda tu kunaweza kufanya mwili wako uwe katika hali inayotakiwa.

Watu wengi wanatumia chakula cha wanga mwingi wakati wa usiku, muda ambao wanakwenda kulala na ziada ya chakula haifanyi kazi vizuri zaidi ya kujikusanya, kujibadilisha na kuhifadhiwa katika maeneo mbalimbali ya mwili hasa tumboni na kwenye makalio.

Mazoezi ya viungo husaidia kuchoma mafuta ya ziada katika mwili. Wanaume huwa na asilimia 8 hadi 20 ya mafuta katika mwili na wanawake ni asilimia 13 hadi 25.

Unapofanya mazoezi ya viungo unaongeza hewa ya oksijeni katika mapafu na wakati huohuo mwili nao unaunguza mafuta ili kutoa nguvu kwa mwili. Kwa ushauri zaidi wasiliana na daktari.
Tupia Comment Yako